KAMPENI YA USALAMA BARABARANI YA“WAIT TO SEND”YAWAFIKIA MADEREVA MBEYA‏

Ofisa wa Jeshi la Polisi – Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Mbeya Mkunde Said (kushoto)akimpima kiwango cha pombe mwilini dereva wa basi la kwenda mikoani, Fikiri Sabigo kwa kutumia kifaa maalum wakati wa upimaji madereva ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni ya Usalama Barabarani ya”Wait to Send” unaohamasisha madereva wa vyombo vya moto kutokutumia simu za mkononi wakati wakiwa wanaendesha vyombo hivyo.Katikati ni Mkuu wa Vodacom Tanzania kanda ya Nyanda za juu kusini Macfadyne Minja Zoezi hili lilifanyika leo katika kituo kikuu cha mabasi mkoani Mbeya yaendayo mikoani katika mwendelezo wa kampeni hiyo inayofanyika nchi nzima na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.
Dereva wa mabasi yaendayo mikoani Mohamed Shaban(kushoto)akipimwa kiwango cha pombe mwilini na Ofisa wa Jeshi la Polisi – Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Mbeya,Mapunda Ahmed(kulia)kwa kutumia kifaa maalum wakati wa upimaji madereva ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa kampeni ya Usalama Barabarani ya”Wait to Send” unaohamasisha madereva wa vyombo vya moto kutokutumia simu za mkononi wakati wakiwa wanaendesha vyombo hivyo.Katikati ni Nashon Mudala mtaalam wa usalama na Afya na mazingira wa Vodacom Tanzania.Zoezi hili lilifanyika leo katika kituo kikuu cha mabasi mkoani Mbeya yaendayo mikoani katika mwendelezo wa kampeni hiyo inayofanyika nchi nzima na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania.

No comments:

Post a Comment