Dar
es Salaam. Hatima ya mawaziri na watendaji waliotajwa katika sakata la uchotwaji
wa Sh306 bilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow itajulikana Jumatatu ijayo
wakati Rais Jakaya Kikwete atakapohutubia taifa kupitia mazungumzo na wazee wa
Mkoa wa Dar es Salaam.
Hotuba
hiyo ya Rais Kikwete inafanyika ikiwa imepita wiki moja iliyopangwa kukamilisha
uchambuzi na kutoa uamuzi dhidi ya wahusika.
Hatua
hiyo ya kusogeza mbele muda wa Rais Kikwete kuzungumzia suala hilo inazidi
kuwaweka tumbo joto mawaziri na viongozi wengine wanaotuhumiwa kuhusika katika
sakata hilo.
Taarifa
za awali zilizotolewa na vyombo kadhaa vya habari zilieleza kuwa Rais Kikwete
angezungumza jana alasiri, lakini Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ilikanusha na
kutoa taarifa nyingine, ikieleza kuwa atazungumza Jumatatu.
No comments:
Post a Comment