Mawaziri, ma-DC, viongozi wa Serikali matumbo joto


Dar es Salaam. Hatima ya mawaziri na watendaji waliotajwa katika sakata la uchotwaji wa Sh306 bilioni katika Akaunti ya Tegeta Escrow itajulikana Jumatatu ijayo wakati Rais Jakaya Kikwete atakapohutubia taifa kupitia mazungumzo na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Hotuba hiyo ya Rais Kikwete inafanyika ikiwa imepita wiki moja iliyopangwa kukamilisha uchambuzi na kutoa uamuzi dhidi ya wahusika.
Hatua hiyo ya kusogeza mbele muda wa Rais Kikwete kuzungumzia suala hilo inazidi kuwaweka tumbo joto mawaziri na viongozi wengine wanaotuhumiwa kuhusika katika sakata hilo.
Taarifa za awali zilizotolewa na vyombo kadhaa vya habari zilieleza kuwa Rais Kikwete angezungumza jana alasiri, lakini Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ilikanusha na kutoa taarifa nyingine, ikieleza kuwa atazungumza Jumatatu.

No comments:

Post a Comment