Wahitimu 344 darasa la saba hawajui kusoma wala kuandika


Arusha. Wanafunzi 344 waliomaliza darasa la saba mwaka huu mkoani hapa wamebainika kuwa hawajui kusoma, kuandika na kuhesabu. Ofisa elimu wa mkoa, Nestory Mloka alitoa taarifa hiyo juzi katika kikao cha elimu kilichoitishwa kwa ajili ya kuchambua matokeo ya mtihani wa darasa la saba na kuwapangia shule wahitimu waliofaulu.

Mloka alisema kati ya walihitimu hao ambao hawajui kusoma na kuandika, wavulana ni 163 na wasichana 181.

Alisema Wilaya ya Ngorongoro yenye wakazi wengi wafugaji wa jamii ya Kimasai, ndiyo ina idadi kubwa ya wanafunzi hao wenye tatizo hilo wanaofikia 230.

No comments:

Post a Comment