Waziri Mahanga anusurika kipigo.

Polisi wamuokoa chini ya ulinzi mkali, Wananchi wamzomea, wamwita mwizi.

Mbunge wa jimbo la Segerea wilayani Ilalal, mkoa wa Dar es Salaam, Dkt. Makongoro Mahanga, akiondolewa na askari polisi kwenye ukumbi wa Anatouglou, Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam leo Jumatano Januari 7, 2014, baada ya kundi la watu wenye "jazba', kutishia kumpa kichapo kama asingeondolewa kwenye eneo hiloambalo lilitumiwa kuwaapisha wenyeviti wa serikali za mitaa kutoka wilaya hiyo.
"Atoke, atoke, atoke" hizo ni kelele kutoka kwa watu hawa, huku polisi wakijaribu kuwatuliza
Dkt. Mahanga, akiwa anatoka kwenye ukumbi huo huku polisi wakiwa "hawachezi mbali"
Vurugu katika zoezi la kuapisha wenyeviti wateule wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji zimepamba moto, ambazo zimesababisha Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk. Makongoro Mahanga, kujikuta akizomewa na wananchi na kusababisha zoezi hilo katika baadhi ya mitaa na vitongoji katika maeneo mbalimbali nchini kukwama.

Dk. Mahanga, ambaye pia ni Mbunge wa Segerea (CCM) alikumbwa na masaibu hayo wakati wa hafla ya kuapisha wenyeviti na wajumbe wa serikali za mitaa katika Wilaya ya Ilala, jijini Dar es Salaam na hivyo, kulazimika kuondolewa katika ukumbi wa Halmshauri ya Manispaa ya Ilala wa Anartoglou chini ya ulinzi mkali wa polisi.

Kabla ya kukumbwa na mkasa huo, Dk. Mahanga alifika katika ukumbi huo ili kushuhudia kuapishwa kwa viongozi wa serikali za mitaa wanaotoka katika jimbo lake.

Katika eneo hilo, kulikuwako na mchanganyiko wa watu, wakiwamo wapambe waliokuwa wakishuhudia zoezi hilo.

No comments:

Post a Comment