Phyllis Omido mshindi wa tuzo la Goldman
Phyllis Omido, kutoka Kenya, alikuwa miongoni
mwa washindi sita waliokabidhiwa tuzo hilo huko San Francisco, Marekani,
Jumatatu usiku. Omindo alipata tuzo hilo kwa kutetea wakaazi wa mtaa wa mabanda
wa Owino Ohuru ulioko Mikindani kaunti ya Changamwe mjini Mombasa.
Wakaazi hao wameathirika na sumu aina ya
''lead'' kutokana na kiwanda cha kukarabati betri kuu kuu kilichojengwa karibu
na mtaa huo wa mabanda. Ukarabati wa betri kuu ulisababisha umwagikaji wa madini
ya sumu aina ya "lead" na kuwadhuru kiafya wakaazi hao kiasi kwamba baadhi ya
wanaume sasa wameshindwa kutekeleza majukumu yao ya nyumbani.
Kiwanda hicho kilianza kazi mwaka wa 2009 lakini
Omido alitetea wakaazi hao wa Uwino Uhuru kwa kufanya maandamano ya mara kwa
mara hadi kikafungwa miaka mitatu baadae.
No comments:
Post a Comment