Tahadhari zachukuliwa hofu ya ugaidi

Dar, Mikoani. Ulinzi umeimarishwa kwenye maeneo mbalimbali nchini ikiwamo vyuoni, ofisi za umma na kwenye migahawa mikubwa baada ya kuwapo kwa hofu ya shambulizi la kigaidi katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha na Mwanza.
Hofu hiyo imekuja baada ya hivi karibuni Chuo Kikuu cha Garissa, cha nchini Kenya kushambuliwa na kusababisha vifo vya wanafunzi 148.
Baada ya shambulizi hilo, kumekuwa na ujumbe mfupi wa simu unaoendelea kusambazwa ukionya kuwapo kwa shambulizi katika mikoa ya Mwanza, Arusha na Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment