Kwa nini nimeamua kuandika mada hii? Kwanza ni kile ambacho nimekuwa nikikiona kwenye jamii ninayoishi. Watu kupenda kulazimisha penzi na kuwa tayari kufanya lolote ili wapendwe.
Hilo ni tatizo na ndiyo maana nikaona nitumie kalamu yangu kuwaelimisha watu hao. Pili ni ushuhuda wa mmoja wa wasomaji wangu aliyejitambulisha kwa jina moja la Nadhifa, mkazi wa Arusha ambaye alinipa kisa cha kusikitisha.
Huyu ni msichana ambaye anatokea kwenye familia yenye uwezo kifedha lakini alichokuwa anakikosa ni penzi la kweli kutoka kwa mwanaume aliyempenda.
No comments:
Post a Comment