Bujumbura, Burundi
Polisi mjini Bujumbura leo wamefyatua za moto hewani katika kukabiliana na maandamano mapya ambayo yameanza maeneo kadhaa ya mji huo.
Makundi mbalimbali ya vijana yaliweka vizuizi barabarani huku wakiimba nyimbo za kumtaka Rais Pierre Nkurunziza abadili msimamo wake wa kutaka kugombea awamu ya tatu ya Urais nchini humo.
Maandamano hayo yameanza siku chache baada ya kushindwa kwa jaribio la mapinduzi ya kijeshi dhidi ya serikali ya Nkurunzinza.
No comments:
Post a Comment