KIZIMBANI KWA KUPELEKA WANAWAKE KENYA KUFANYA BIASHARA YA NGONO

Na Kulwa Mzee, Dar es Salaam
WANAWAKE wawili wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za kusafirisha mabinti kutoka Tanzania kwenda Kenya kwa ajili ya kuwafanyisha ngono.

Washtakiwa hao Jackline Milinga (23) na Mary Amukowa (29) ambaye ni Mkenya walifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashtaka ya kuwasafirisha mabinti 10.

Wakisomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Waliarwande Lema na Wakili wa Serikali, Jackline Nyantori na Selestine Makoba walidaiwa kutenda makosa hayo Septemba 4 mwaka huu.
Nyantori alidai washtakiwa kwa pamoja, Septemba 4 mwaka huu maeneo ya Magomeni na Makumbusho waliwaajiri mabinti hao kumi na kuwasafirisha.

No comments:

Post a Comment