Jana Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Manispaa za Jiji la Dar es Salaam, zilianza kazi ya kubomoa nyumba zote zilizo katika maeneo oevu, kando ya mito na bahari.
Mkuu wa Kitengo cha Sheria Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira Tanzania (NEMC), Manchale Heche alisema bomoabomoa hiyo inalenga kuzibomoa nyumba zaidi ya 4,000 zilizojengwa katika maeneo hayo huku nyingi zikiwa ni katika Bonde la mto Msimbazi.
“Leo hapa Jangwani tumeanza kwa kubomoa nyumba zaidi ya 100, lakini nyumba zaidi ya 4,000 zinatarajiwa kubomolewa na hizi ni zile zote ambazo zimejengwa katika maeneo ambayo yanakatazwa kisheria,” alisema Heche.
No comments:
Post a Comment