Kamanda Mpinga akwamisha ulanguzi tiketi Ubungo

2.Kamanda Mpinga akiwa ndani ya Basi la kuelekea Tanga akizungumza na baadhi ya abiria juu ya viwango vya nauli walivyotozwa kama vipo sahihi.Kamanda Mpinga akiwa ndani ya basi la kuelekea mkoani Tanga akizungumza na baadhi ya abiria juu ya viwango vya nauli walivyotozwa kama vipo sahihi.
3.Abiria waliokuwa wakisafiri kuelekea Mkoani Tanga wakimsikiliza kwa Makini kamanda wa polisi kikosi cha usalama barabarani nchini,Mohammed Mpinga.Abiria waliokuwa wakisafiri kuelekea mkoani Tanga wakimsikiliza Mpinga.
4.Kamanda Mpianga na Kamishna Msaidizi wa kanda maalum ya polisi Dar es Samaam, Peter Sima (kushoto) wakiwa ndani ya moja ya basi.Kamanda Mpinga na Kamishna Sima wakiwa ndani ya moja ya mabasi kituoni hapo.
5.Kamanda Mpinga akishuka ndani ya basi stendi ya Ubungo Dar.Kamanda Mpinga akishuka ndani ya basi baada ya kuchukua maoni ya abiria.
6.Abiria wakiwa makini kuhakikisha wanafunga mikanda iliyoko kwenye viti vyao vya kukalia.Abiria wakiwa makini kuhakikisha wanafunga mikanda kwenye viti vya kukalia
7.Kamanda Mpinga (kushoto) akiwa na Kamishna msaidizi wa  kanda maalum ya polisi Dar es alaam, Peter Sima.Kamanda Mpinga (kushoto) akiwa na Kamishna Msaidizi wa Kanda Maalum ya Polisi Dar es alaam, Peter Sima.1.Abiria wakisafiri na mabegi yao katika stendi ya Mabasi ubungo .Abiria wakiwa na mabegi tayari kwa usafiri katika stendi ya mabasi Ubungo.
8.Abiria wakiwa stenda ya Ubungo  kuelekea mikoani kusherehekea sikukuu za Krismas na Mwaka Mpya.Abiria wakiwa stendi ya Ubungo kuelekea mikoani kusherehekea sikukuu za Krismas na Mwaka Mpya.
9.Harakati za hapa na pale kwa abiria walokuwa stendi ya Ubungo Dar zikiendelea.Harakati za hapa na pale kwa abiria zikiendelea.
10.Abiria wakijianda kupanda basi lao kwa ajili ya safari.Abiria wakijianda kupanda basi.
11.Basi zilizokuwa zikifanya safari zake jijini Dar es Salaam zilizopewa vibali vya mda kusafirisha abiria mikoani zikiwa stendi ya Ubungo.Mabasi yaliyokuwa yakifanya safari zake jijini Dar es Salaam yaliyopewa vibali vya muda kusafirisha abiria mikoani yakiwa stendi ya Ubungo.
12.Taswila ya stendi ya ubungo.Taswira ya stendi ya Ubungo ilivyokuwa leo.
KAMANDA wa Polisi Kikosi Cha Usalama Barabarani nchini, Mohammed Mpinga, kwa kushirikiana na Kamishna Msaidizi wa Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, Peter Sima, wameyadhibiti mabasi yaendayo mikoani katika stendi ya Ubungo yasipandishe nauli ambapo ulanguzi wa tiketi kwa abiria ulionekana kugonga mwamba.
Kamanda Mpinga na Kamishna Sima wametembelea ndani ya mabasi na kuuliza baadhi ya abiria juu ya nauli waliyolipia kama ndiyo sahihi kama iliyotangazwa na Mamlaka ya Udhibiti, Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) huku wakisisitiza abiria kufunga mkanda na kutoa taarifa juu ya dereva anayeendesha gari kwa mwendo kasi.
Mpinga amesema, abiria yeyote atakayepandishiwa nauli tofauti na viwango vilivyotangazwa na serikari atoe taarifa kupitia namba maalum zilizotajwa kabla ya kuanza safari yao kuepuka mgogoro unaoweza kujitokeza wawapo safarini huku akizidi kusisitiza kuwa hakuna abiria atakayezidishiwa nauli kwa kipindi hiki cha sikukuu za Krismas na Mwaka mpya wa 2016.
Kwa upande wa askari wa vikosi vya barabarani (trafiki) Kamanda Mpinga amesema wamejipanga kuhakikisha askari wote wanakuwa na tochi maalum za kumulika magari yanayoendeshwa kwa mwendo kasi ili kupunguza hatari dhidi ya abiria.
(NA DENIS MTIM A/GPL)

No comments:

Post a Comment