Miongoni mwa mafanikio yanayompa sifa Rais Dk. Magufuli, ni kuweka rekodi kubwa ya kukusanya ndani ya muda mfupi, inayokadiriwa kufika Sh.trilioni 1.3 ndani ya mwezi mmoja, kudhibiti wizi wa fedha za serikali na kubana bajeti.
Kiongozi huyo aliyekabidhiwa nafasi hiyo Novemba 5, mwaka huu, licha ya kioo bora cha mafanikio aliyoyaonyesha, pia anakabiliwa na changamoto ya kutekeleza ahadi kuu sita alizozitoa wakati wa kampeni, ambazo ni zifuatazo:
Ujenzi wa Mahakama ya Mafisadi
Ni ahadi aliyokuwa akiitoa kwamba angeitekeleza mara moja, pindi angechaguliwa kushika madaraka aliyo nayo sasa.
Katika moja ya mikutano yake, Rais Dk. Magufuli, katika mikutano yake ya kampeni, alikuwa kila mara alikuwa akirudia matashi: “Nitasimamia uundwaji Mahakama ya Kushughulikia Mafisadi na ‘Majizi’ wa nchi ili wafungwe.”
No comments:
Post a Comment