Meneja Mkuu Kiwanda cha Urafiki asimamishwa kazi.

Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara, imeingilia kati mgogoro wa Kiwanda cha Nguo cha Urafiki kwa kuwasimamisha kazi Meneja Mkuu wa kiwanda hicho, Nassoro Baraza na Naibu Meneja Mkuu, Samweli Swai ili kupisha uchunguzi dhidi yao ufanyike na endapo watabainika kuwa ni chanzo cha mgogoro huo watachukuliwa hatua za kisheria.

Aidha, serikali imetoa miezi sita kwa kiwanda hicho kiwe kimewalipa wafanyakazi madai yao mbalimbali sambamba na kuanza kulipa nyongeza ya mishahara wanayodai kama sehemu muhimu ya kumaliza kabisa mgogoro huo.

Akitoa agizo hilo jana, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Uledy Mussa, alisema serikali imeona ni vema kufanya maamuzi magumu kwa mtu mmoja au wawili ili kunusuru uwapo wa nguvu kazi nyingi hasa kwa watu wanaohitaji kutimiziwa haki zao za msingi.

No comments:

Post a Comment