Uporaji wa fedha kwa bodaboda watikisa Dar

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura

Matukio ya uporaji na mauaji kwa kutumia pikipiki yanazidi kushika kasi na kusababisha hofu kubwa kwa wananchi na wafanyabiashara jijini Dar es Salaam pindi wanapotoka benki, wanaposafirisha fedha kutoka eneo moja kwenda jingine au kufanya manunuzi.

Uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa, uporaji huo unaofanywa na majambazi kwa kutumia pikipiki hasa aina ya Boxer una mtandao mkubwa wa wahusika kutoka hatua ya kwanza ya mtu anapochukua fedha iwe benki au sehemu nyingine yeyoye hadi tukio zima la kuporwa linapotokea.

Jana watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi katika eneo la Mikocheni, jijini Dar es Salaam walimuua Conrad Kamukara, kwa kumpiga risasi akiwa anaelekea ofisi za kampuni ya Nabaki Afrika kununua vifaa vya ujenzi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, alithibitisha kutokea kwa tuki hilo na kusema watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakiwa kwenye pikipiki walimvamia kijana huyo na kumpiga risasi na kumuua.
Kamanda Wambura alisema kabla ya tukio hilo kutokea, Kamukara alikuwa akiongea na ndugu zake kwa simu kuwa ataelekea Nabaki Afrika kununua vifaa vya ujenzi vikiwamo vigae.

No comments:

Post a Comment