Polisi Dar wasaka majambazi benki

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema kuwa wapo baadhi ya wafanyakazi wa benki, ambao kwa namna moja au nyingine, wanashirikiana na majambazi kufanya uhalifu; na sasa linawasiliana na wamiliki wa taasisi za kifedha, kujiridhisha uhusika wao na uhalifu wa kutumia silaha.

Aidha, limesema mtu yeyote atakayetaka kusindikizwa na polisi kwenda kuchukua fedha nyingi benki, anaruhusiwa kwa kulipia Sh 10,000 au Sh 20,000.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda hiyo, Simon Sirro alisema wameanza kuweka ulinzi mkali katika benki mbalimbali, ikiwemo zilizopo eneo la Mlimani City na kwamba wanakagua pikipiki na watu wanaowatilia shaka.

No comments:

Post a Comment