Kiama cha mafisadi.

Sasa ni dhahiri kiama cha mafisadi kimetimia baada ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuwasilisha bungeni mapendekezo mbalimbali ili kuipa meno zaidi ya kuchunguza na kufuatilia mali zinazomilikiwa na watumishi wa umma isivyo halali.

Hatua hii imelenga katika kuhakikisha kwamba Serikali ya Rais Dk. John Magufuli, inawashughulikia mafisadi kikamilifu.

Aidha, mapendekezo hayo yanalenga kufanya marekebisho ya vifungu 16 ambavyo vipo kwenye vipengele vitatu vya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Namba 13 ya mwaka 1995, ambayo kwa kiasi kikubwa haikutoa nguvu za kisheria kwa Sekretarieti kutekeleza majukumu yake kwa uhuru.

No comments:

Post a Comment