MAKAME MBARAWA - MUDA WA UZIMAJI SIMU FEKI HAUTAONGEZWA

Waziri  wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiiano Profesa Makame  Mbarawa amesema Serikali haitaongeza muda katika zoezi zima la uzimaji wa simu feki ifikapo Juni 16 mwaka huu.

Ameyasema hayo ofisini kwake leo jijini Dar es salaam wakati wa mahojiano na kituo kimoja cha habari hapa nchini.

Amesema Serikali imeamua kuchukua uamuzi huo kutokana na madhara mbalimbali yatokanayo na simu hizo ikiwemo ya kiafya na kusisitiza kuwa serikali inapoteza mapato mengi kutokana na uingizwaji wa simu hizo nchini.

"Tunategemea kuzima simu zote feki kutokana na madhara yake kiafya  hasa kwa watumiaji, kukosekana kwa viwango vya ubora wa simu hizi na hivyo wananchi kupoteza fedha nyingi kwa ajili ya ununuzi wa simu hizi kwani hufa mara kwa mara", amesema Waziri Mbarawa.

No comments:

Post a Comment