Inaweza kuwa hospitali bora kuliko zote za Serikali nchini ikiwa na kila aina ya wauguzi waliobobea, vifaa tiba na dawa, lakini Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) yaweza kufananishwa na tanuru la moto kwa wajawazito kwenye baadhi ya wodi.
Muhimbili inahudumia wagonjwa wa aina zote, wengi wakiwa waliopewa rufaa kutoka hospitali za jijini Dar es Salaam na mikoa mingine na hupata huduma kwa madaraja kulingana na uwezo wao, lakini wale wa kiwango cha chini ndio ambao hulazimika kustahimili kila aina ya vitendo visivyo na staha kutoka kwa baadhi ya wahudumu.
Baadhi hujiona kama wanazidishiwa magonjwa na wengine au watoto waliowazaa kwa njia ya upasuaji hupoteza maisha kutokana na huduma zisizo na ubora kutoka kwa baadhi ya wahudumu.
Mwandishi wa gazeti hili (jina tunalihifadhi) alishuhudia vitendo hivyo wakati alipokuwa kwenye wodi namba 33 ya MNH ambayo inahudumia wanawake wengi wanaojifungua kwa njia ya upasuaji.

No comments:
Post a Comment