Mwenye mishahara hewa 17 TRA aonja joto ya jiwe

Rais Magufuli alifichua uwapo wa mfanyakazi huyo hivi karibuni akiwa nyumbani kwake katika Kijiji cha Mlimani, Wilaya ya Chato mkoani Geita, alipokuwa akihutubia kwa mara ya kwanza nyumbani kwake tangu aapishwe kuwa Rais Novemba 5, mwaka jana.

“Yupo mfanyakazi mmoja wa TRA ambaye alikuwa akilipwa mishahara ya watu 17 na huyo ni lazima afikishwe mahakamani,” alisema Rais Magufuli akiwa nyumbani kwake wilayani Chato.

Gazeti hili limefuatilia hatua ambazo TRA imechukua tangu Rais amfichue mtumishi huyo na kuambiwa ameanza kushughulikiwa na kila kitu kitawekwa wazi mambo yatakapokamilika.

“Rais akisema vile ni agizo,” kilisema chanzo kimoja kutoka ndani ya Mamlaka hiyo, "hivyo huyo mtu atafikishwa mahakamani.

No comments:

Post a Comment