WAGOMBEA URAIS 11 CCM WAPEWA KAZI SERIKALINI

Rais John Magufuli amemteua Mathias Chikawe kuwa Balozi wa Tanzania nchini Japan.
Huu ni mwendelezo wa kuwakumbuka kwa kuwapangia majukumu ya kitaifa baadhi ya makada wa CCM waliopambana naye katika mbio za kuwania nafasi ya urais kupitia chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.
Kabla ya kupangiwa kituo hicho cha kazi, Chikawe aliteuliwa kuwa balozi Februari 15, mwaka huu sambamba na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi wa Taifa (NSSF), Dk Ramadhani Dau na Dk Asha-Rose Migiro.
Chikawe, ambaye ameanza kutekeleza majukumu yale tangu Aprili 13, alikuwa miongoni mwa makada 38 wa CCM waliochukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi ya urais kwa tiketi ya CCM.

Makada waliokumbukwa
Makada wengine waliokumbukwa katika Serikali ya Magufuli ni Profesa Sospeter Muhongo, Dk Harrison Mwakyembe, January Makamba, Mwigulu Nchemba, Dk Khamis Kigwangalla, Balozi Augustino Mahiga na Dk Asha-Rose Migiro.

No comments:

Post a Comment