AMUUA MKEWE, ACHOMA NYUMBA MBILI

Kamanda wa Polisi Tarime Rorya, ACP Andrew Satta.

MKAZI wa kitongoji cha Nyabirama kijiji cha Matongo Nyamongo, Tarafa ya Ingwe, wilayani Tarime mkoani Mara Wambura Mrimi (50) amepata kipigo kutoka kwa wananchi na kulazwa akiwa na hali mbaya kwa tuhuma za kumchinja kwa kumkata shingo mke wake Maria Maningo (38) na kuchoma nyumba zake mbili baada ya kumhusisha mke wake na imani za kishirikina.

Mrimi amelazwa katika Hospitali ya wilaya Tarime akiwa chini ya ulinzi mkali. Kamanda wa Polisi Tarime Rorya, ACP Andrew Satta alisema kuwa tukio hilo la mauaji lilifanyika June 8, mwaka huu katika kitongoji cha Nyabirama, kijiji cha Matongo Nyamongo baada ya kutokea ugomvi kati ya mke na mume.

No comments:

Post a Comment