KAMPUNI YA KIGENI INAPOTUMIA MBINU CHAFU KUDHALILISHA SERIKALI


Gari la Kampuni ya Wengert Windrose Safaris likiwa limeshikiliwa kituo cha polisi mkoani Arusha baada ya kukutwa na shehena ya bangi.

Na Mwandishi Wetu

BIASHARA ya utalii imekuwa na ushindani mkubwa si nje bali hata ndani ya nchi yetu. Ushindani wa kibiashara unadhihirishwa na jinsi ambavyo makampuni ya ndani na nje yanavyopigana vikumbo kutafuta njia na mbinu za kuwapiku washindani wao.

Hilo ni jambo la kawaida kabisa.

Hakika pale ambako hapana ushindani basi ni wazi pia kwamba hapatakuwapo na tija kwani mama wa biashara huria ni ushindani na hilo hakuna wa kubishana. Hata hivyo, kuna mvutano ambao umeanzishwa na kampuni ya Wengert Windrose Safaris Limited, kampuni tanzu ya Friedkin Conservation Fund (Friedkin Family Tanzania) dhidi ya serikali ya Tanzania ambao hauna tija kwa pande zote mbili na ambao unahitaji kumalizwa kwa sababu umeendelea kuikosesha nchi mapato.

No comments:

Post a Comment