WANAFUNZI 316 WALIOFUKUZWA CHUO KIKUU CHA ST. JOSEPH WAFUNGUA KESI MAHAKAMANI

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetoa kibali cha kufungua kesi ya uwakilishi, kwa wanafunzi wanne, waliofukuzwa katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph kwa madai ya kutokuwa na sifa za kudahiliwa kwenye vyuo vikuu.

Jaji Eliezer Feleshi alitoa kibali hicho baada ya wanafunzi hao kuwasilisha maombi ya kibali cha kuwakilisha wenzao mahakamani pamoja na kusitisha masomo wakati kesi ya msingi ikiendelea kusikilizwa.

Wanafunzi hao, walisimamishwa masomo baada ya kutolewa amri ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Joyce Ndalichako kwamba kutokana na tatizo la ufundishaji wa Stashahada ya Elimu (Sayansi, Hisabati na Teknolojia) wanafunzi wote wanatakiwa kurejea nyumbani.

No comments:

Post a Comment