Dar es Salaam. Msichana aliyepooza mwili wake, Wakonta Kapunda ambaye ni miongoni mwa waandishi wa miswada ya filamu waliochaguliwa katika tamasha la Maisha Film Lab lililofanyika siku chache zilizopita visiwani Zanzibar anaomba msaada ili kukamilisha ndoto zake za kuwa ‘daraja’ kati ya jamii na Serikali.
Wakonta alipooza baada ya kugongwa na gari akiwa katika maandalizi ya mahafali ya kidato cha sita ya Shule ya Sekondari ya Wasichana Korogwe mkoani Tanga.
Wakonta alisema jana kuwa anashindwa kumudu gharama za uchunguzi wa maendeleo ya afya yake na matibabu kwa kukosa fedha.
“Watu wanaopata matatizo kama yangu huwa katika wakati mgumu kutokana na kuchelewa kupona, nahitaji uangalizi wa karibu wa daktari na changamoto inayonikabili ni fedha,” alisema.
No comments:
Post a Comment