MAHAKAMA Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, imetoa masharti ya dhamana kwa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu na wenzake watano, wanaokabiliwa na mashitaka ya kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 1.2.
Jaji Eliezer Feleshi, alitoa masharti hayo juzi baada ya kukubali hoja za maombi yaliyowasilishwa na washtakiwa hao. Hata hivyo baada ya kutolewa kwa masharti hayo, washtakiwa walirudishwa rumande baada ya kushindwa kuyatimiza.
Mbali na Maimu, washtakiwa wengine waliopewa masharti ya dhamana ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), Joseph Makani, aliyekuwa Ofisa Usafirishaji, George Ntalima, na aliyekuwa Mkurugenzi wa Sheria, Sabina Raymond.
Wengine ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Bima ya Aste Insurance Brokers Company, Astery Mwita Ndege, aliyeingia mkataba na Nida wa kutoa huduma za bima na Xavery Silverius Kayombo, ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Gotham Internatianal Limited.

No comments:
Post a Comment