MATAPELI WAVAMIA DAR, KAMANDA SIRRO AWATAKA WANANCHI KUWA MAKINI

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam leo limetahadharisha wananchi wa Jiji hilo kuwa kuna wimbi la matapeli wanaotumia ukosefu wa ajira kama njia ya kutapeli wananchi.
Kamishna wa Kanda hiyo, Kamanda Simon Sirro amesema jeshi la polisi lilipokea taarifa kutoka kwa raia mwema ambaye alitapeliwa na watu hao.
Sirro amefafanua kuwa, matapeli hao huwarubuni watu kuwa wana kampuni zinazohusika na kutafutia watu ajira na kwamba hutoa masharti kwa anayehitaji ajira kulipia baadhi ya gharama kwa ajili ya kulipa watu wanaohusika na usaili wa kazi hizo.
Amewataka wakazi wa jiji la Dar es Salaam kuwa makini na kwa mwenye taarifa sahihi za matapeli hao kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa zao katika vituo vya polisi.

No comments:

Post a Comment