PROGRAMU YA BAHATI NASIBU YA VIZA YA UKAAZI WA KUDUMU MAREKANI IMEANZA


Ubalozi wa Marekani 
Dar es Salaam 
TANZANIA
13 Oktoba, 2016





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
PROGRAMU YA BAHATI NASIBU YA VIZA YA UKAAZI 
WA KUDUMU MAREKANI IMEANZA

Ubalozi wa Marekani jijini Dar es Salaam unatangaza kuanza kwa programu ya Bahati Nasibu ya Viza ya Ukaazi wa kudumu Marekani (Diversity Visa Program) kwa mwaka 2018 (DV-2018).  Kila mwaka, kupitia programu hii, Marekani hutoa viza za ukaazi wa kudumu (immigrant visas) zipatazo 55,000 kwa raia wa nchi ambazo kihistoria zina idadi ndogo ya watu wanaohamia Marekani. Mwaliko unatolewa kwa Watanzania wenye sifa kutuma maombi yao katika programu hii ya uhamiaji kabla ya tarehe 7 Novemba 2016.
Tafadhali soma kwa makini na kwa ukamilifu maelekezo ya namna ya kutuma maombi yako katika tovuti maalumu ya Masuala ya Uhamiaji katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani inayopatikana katika anuani ifuatayo; www.dvlottery.state.gov.  Maombi ya kupata viza hiyo katika kipindi cha mwaka 2018 (DV-2018) yanapokelewa hivi sasa hadi tarehe 7 Novemba 2016 saa.  Unaweza kutuma ombi lako mara moja tu na kwa njia ya mtandao pekee.  Maombi hayatapokelewa kwa njia ya barua wala kuletwa kwa mkono.

No comments:

Post a Comment