Wanafunzi wasoma chini ya miembe

SHULE ya Msingi Kashifa, kata ya Ikola, iliyo mwambao mwa Ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Tanganyika, mkoani Katavi, inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa na kusababisha wanafunzi kusoma chini ya miti kwa zaidi ya miaka mitano.

Shule hiyo yenye zaidi ya wanafunzi 600 wanaosoma kuanzia darasa la kwanza hadi la saba ina vyumba viwili vya madarasa.

Akizungumza na gazeti hili, diwani wa Ikola, Philiomon Moro alikiri kuwa shule hiyo inakabiliwa na uhaba wa vyumba vya madarasa. Alisema vyumba vipo viwili hivyo walimu wanalazimika kufundisha wanafunzi wakiwa wameketi chini ya miembe.

No comments:

Post a Comment