Na Dorine Otinga, Nairobi
JE, hatima ya Kenya katika uchaguzi wa 2017 ni ipi? Hili ni swali sugu ambalo kila Mkenya anasubiri jibu lake kwa hamu. Uchaguzi wa urais ndio uti wa mgongo wa maendeleo ya nchi yoyote. Ni ndoto ya kila mmoja kuishi katika maeneo yenye haki, usawa na amani. Kenya inapitia hatua muhimu inapojiandaa katika uchaguzi wa urais wa 2017.
Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC)
Hii ni tume ambayo hujihusisha na shughuli za kuhesabu kura katika uchaguzi nchini Kenya. Mnamo Mei mwaka huu, kulikuwa na ghasia zilizotokana na maandamano katika mji mkuu wa Nairobi na kusababisha vifo vya watu watatu.
Maandamano haya yalisababishwa na wafuasi wa chama cha CORD ambacho kinara wake ni Raila Odinga. Sababu kuu ya maandamano hayo, ni kwamba walitaka serikali ifanye mabadiliko katika tume hii ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).
No comments:
Post a Comment