KUCHANGANYA POMBE NA VINYWAJI VYA KUONGEZA NGUVU (ENERGY DRINKS) NI HATARI KWA AFYA YAKO


Mchanganyiko wa pombe na vinywaji vya kuongeza nguvu vijulikanavyo kama Energy drinks vilitosha kumfanya akose usingizi na kuwa mwenye nguvu kwa muda wote kipindi alipokuwa akikesha katika kumbi tofauti tofauti za starehe katika katika jiji la Dar es Salaam wakati akisoma katika chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Lakini leo hii akizungumzia mambo yanayohusu afya yake na yako, kuchanganya pombe na Energy drinks ni jambo ambalo asingekushauri kabisa ulifanye. Kwani hali ya afya yake ipo ukingoni na asingependa kabisa kuona mtu mwingine akiingia katika majanga aliyoyapata yeye.
Je ni kweli vinywaji hivi vijulikanavyo kwa jina la energy drinks huongeza nguvu kama inavyosemekana? Wataalam wa afya wanatoa tahadhari kuhusiana na madhara yatokanayo na hivi vinywaji maarufu. Utumiaji wa vinywaji hivi kwa muda mrefu husababisha matatizo ya moyo ambayo ni hatari sana kwa afya yako.


No comments:

Post a Comment