Dar es Salaam. Zikiwa ni siku nne tangu kuuawa na polisi kwa kupigwa risasi, Salum Almasi akituhumiwa kuwa ni jambazi, ndugu zake hawajamzika wakisema mazingira ya kifo chake yana utata.
Mei 14, nje ya jengo la Makao Makuu ya Idara ya Uhamiaji, Kurasini jijini hapa, Almasi aliuawa akidaiwa pamoja na wenzake walifanya jaribio la kupora fedha wakati gari likizipeleka kwenye mashine ya kielektroniki ya kutolea fedha (ATM) iliyopo kwenye jengo hilo.
Akizungumza jana, msemaji wa familia, Tulleyha Abdulrahman ambaye ni mjomba wa Almasi, alisema utaratibu wa maziko haujakamilika na kwamba, wanashangazwa na tuhuma zinazotolewa dhidi ya ndugu yao kwamba ni jambazi.
No comments:
Post a Comment