Sijaelewa tafsiri ya uongo kwangu iko wapi – Ruge Mutahaba

Mkurugenzi na mzalishaji wa vipindi waClouds Media Group, Ruge Mutahaba, ameijibu kauli iliyotolewa na Mkuu wa mkoa wa Dar Dar es salaam, Paul Makonda ya kuwa yeye ni muongo, na anafaa tu kuwa muandishi wa mashairi na nyimbo za mapenzi na ngonjera.

Ruge ametoa kauli hiyo leo katika kipindi cha Clouds 360 kinachorushwa na kituo hicho, ambapo walikuwa na kipindi cha ‘SHUKRANI’ kwa wasikilizaji wao na watu waliowahi kuwasaidia kupata misaada.
“Kila mtu ana mtazamo wake, na huwezi kulazimisha mtazamo wa mtu ubadilike. Inasikitisha sana kuona mtu anayesambaza haya mambo ni bosi wangu, Bosi wa mkoa wetu. Yeye akipiga mhuri kitu ndio imekaa hiyo, Yeye ana nguvu zote,” amesema Ruge.

No comments:

Post a Comment