
Soko la Kampochea lililopo Mbagala Rangi Tatu jijini Dar es Salaam limeteketea kwa moto alfajiri ya leo Jumanne Machi 6, 2018 na kusababisha hasara kwa wafanyabiashara wa eneo hilo.
Imeelezwa moto huo ulianza kuteketeza mabanda ya soko hilo saa 12 alfajiri huku uongozi ukitaja kuwa chanzo ni hitilafu ya umeme.

Mwenyekiti wa soko hilo, Mohamedy Njiwa amesema limekuwa likikumbwa na hitilafu za mara kwa mara licha ya kuripoti kwa mamlaka husika.
"Wiki mbili zilizopita hapa kulikuwa na hitilafu ya umeme, ulikuwa unakuja na kukata. Tanesco walikuja kufanya ukaguzi wakaeleza kuwa kuna hitilafu kwenye transfoma,"amesema.
No comments:
Post a Comment