Tanzania yapoteza Sh800 bilioni kwa mwaka


Dar es Salaam. Tanzania imepoteza kiasi cha Dola 462 milioni za Marekani (sawa na Sh794.6 bilioni) mwaka 2013 kutokana na rushwa, udanganyifu katika ankara za malipo na ukwepaji wa kodi.
Shirika la Kimarekani la Uchumi (GFI) limetoa ripoti mpya na kusema kuwa Tanzania imepoteza jumla ya Dola 1,762 milioni kuanzia mwaka 2011 hadi 2013.
Ripoti hiyo iliyotolewa Desemba mwaka huu, inaonyesha kuwa Tanzania imekuwa sugu kwa kupoteza kiasi kikubwa kila mwaka na kwa mwaka 2010, kiasi cha Dola 1,356 milioni kilipotea wakati Dola 613 milioni zilipotea mwaka 2011 na Dola 717 milioni mwaka 2012.
Waziri wa Fedha, Saada Mkuya alisema tatizo la udanganyifu katika ankara za malipo ndilo lililotawala zaidi nchini na kusema linafanyiwa kazi na mamlaka husika.
Mkuya alisema Tanzania inapoteza fedha nyingi zaidi kutokana na udanganyifu katika ankara za malipo ya kibiashara, mchezo ambao umekuwa ukifanywa na raia wa China ambao ankara zao za malipo huonyesha kuwa wameingiza mzigo mkubwa nchini lakini ukifika katika Bandari ya Dar es Salaam, huonekana mzigo kidogo.

No comments:

Post a Comment