Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma, Mihayo
Msikhela akiwaonesha wandishi wa habari ujumbe ulioachwa na marehemu Emmanuel
Moshi baada ya kumuua mfanyabiashara mwenzake Didas Alphonce kwa kumkata na
shoka kichwani na kisha yeye kujiua kwa kujinyonga. Picha Joyce Joliga
Songea. Mfanyabiashara
wa mbao Manispaa ya Songea, Emmanuel Moshi (40), mkazi wa Marangu, mkoani
Kilimanjaro amemuua mfanyabiashara mwenzake aliyetambuliwa kwa jina la Didas
Alphonce (64), mkazi wa Kilema Kilimanjaro kwa kumpasua kichwa kwa shoka, kisha
yeye mwenyewe kujinyonga kwa kutumia kamba ya katani katika stoo ya nyumba
waliyokuwa wakiishi.
Inadaiwa
kuwa Moshi alichukua uamuzi huo baada ya Alphonce kumdhulumu zaidi ya Sh87.4
milioni.
Wakizungumza
na gazeti hili jana, watu wa karibu na wafanyabiashara hao ambao hawakupenda
majina yao kuandikwa kwenye gazeti, walidai kuwa wafanyabiashara hao walikuwa
wakiishi nyumba ya ndugu yake, Didas na kufanya biashara za kuuza mbao
pamoja.
No comments:
Post a Comment