Kashfa ya Tegeta Escrow: Vigogo wawili Serikalini kizimbani

Watuhumiwa wa kesi ya kupokea rushwa kutoka kwenye akaunti ya Tegeta Escrwo, Rugonzibwa Mujunangoma (kushoto) na Theophil Bakwea na wakiingia katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kwa ajili ya kufunguliwa mashitaka. Picha na Said Khamis

Dar es Salaam. Miezi michache baada ya kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow kutikisa nchi, watumishi wawili waandamizi wa Serikali wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakituhumiwa kupokea rushwa ya mamilioni ya fedha zilizotoka kwenye akaunti hiyo.
Mahakama hiyo ilielezwa jana kuwa Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Rugonzibwa Mujunangoma aliwekewa kiasi cha Sh323 milioni kupitia akaunti yake namba 00120102602001.

No comments:

Post a Comment