Polisi yaua majambazi hatari Arusha

WATU watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi ambao ni raia wa Kenya pamoja na Mtanzania mmoja wameuawa katika mapambano na polisi yaliyotokea eneo la Chekereni mpakani mwa wilaya ya Arumeru na Jiji la Arusha.

Aidha majambazi hao wamekufa baada ya jambazi mmoja Sixtus Ngowi (51) ambaye alikamatwa awali kutoa ushirikiano kwa polisi kuwa anashirikiana na wenzake hao watatu raia wa Kenya.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini hapa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema polisi walipokea taarifa za Kiintelijensia Agosti 19, mwaka huu juu ya kuwepo kwa kundi la majambazi wanaotoka Kenya na wamefika mkoani humo kwa lengo la kufanya uporaji kwa kushirikiana na majambazi wenzao wa hapa nchini.

No comments:

Post a Comment