
Taarifa iliyotolewa jana na MCC ilieleza kuwa mkutano wa robo ya mwaka wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika hilo linalomilikiwa na serikali ya Marekani kwa ajili ya kutoa misaada kwa nchi zinazoendelea ulijadili pendekezo la mkataba mpya na serikali ya Tanzania wenye thamani ya dola za Kimarekani milioni 472.8 na kuamua kuwa fedha hizo zitolewe baada ya Tanzania kutimiza kigezo cha kuzuia rushwa. Ilielezwa kuwa msaada huo ni maalum kwa ajili ya kuimarisha sekta ya umeme nchini, lengo likiwa ni kuwawezesha Watanzania wengi zaidi kupata nishati hiyo kwa uhakika na kwa bei nafuu.
Kadhalika, ilieliezwa kuwa msaada huo ungehusisha pia uimarishaji wa taasisi zinazohusika na usambazaji wa umeme na usimamizi wake, kusaidia utekelezaji wa mipango ya mageuzi katika sekta ya nishati na kuchochea uwekezaji wa sekta binafsi.
No comments:
Post a Comment