Bomoabomoa wakati wowote Morogoro

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya
By Lilian Lucas,Mwananchi
Morogoro. Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula amewataka wananchi waliojenga maeneo yasiyo rasmi na wasio na vibali maalumu kuondoka kabla hatua za kisheria hazijachukuliwa dhidi yao.

Kadhalika waziri huyo amesema ni vyema wakazi hao wakaanza kuondoka mapema ili kuondokana na lawama zinazoweza kujitokeza pindi bomoabomoa itakapoanza wakati wowote mkoani Morogoro.

Mabula alitoa kauli hiyo akiwa katika ziara ya kukagua shughuli zinazoendeshwa na wizara hiyo mjini hapa.

Alisema Serikali inahitaji kuona wananchi wanaishi katika maeneo salama na uamuzi wa kuwataka kuondoka mapema katika maeneo hayo unalenga kuwaepusha na majanga yanayoweza kujitokeza kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

No comments:

Post a Comment