Moshi. Nyumba za kifahari zaidi ya 160 za vigogo wa taasisi za Umma na wastaafu katika Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro zinatarajiwa kubomolewa kutokana na kujengwa maeneo ya hifadhi ya vyanzo vya maji.
Nyumba hizo zimejengwa ndani ya mita 60 katika mto Karanga kuanzia eneo la Shanty Town na mto Rau huku nyingine zikijengwa katika vyanzo vya maji kata ya Njoro.
Miongoni mwa nyumba zinazotajwa kujengwa ndani ya mita 60 ni za kigogo mmoja mstaafu wa Jeshi la Polisi, wafanyabiashara mashuhuri na nyingine ujenzi wake ukianza.
No comments:
Post a Comment