
Hatua ya Rais John Magufuli kutaka kupunguza mishahara ya watendaji mbalimbali wa taasisi za umma kutoka kiwango cha juu cha Sh. milioni 40 kwa mwezi hadi kufikia Sh. milioni 15 inatajwa kuwa ni pigo jingine kwa baadhi ya vigogo hao ambao hivi sasa wanateseka kwa kuishi maisha wasiyoyazoea ya kubana matumizi kila uchao.
Rais Magufuli mwenyewe alitangaza katikati ya wiki kuwa anapokea Sh. milioni 9.5 kwa mwezi, kiwango ambacho ni chini ya mshahara wa wabunge wa Sh. milioni 11.9 kabla ya makato.
Akiwa mapumzikoni mkoani Geita katikati ya wiki, Rais Magufuli alisema atapunguza mishahara mikubwa wanayolipwa wakuu wa taasisi za umma ili kuendana na dhamira ya serikali yake ya kujielekeza zaidi katika kuinua hali za wananchi na kwa kufanya hivyo, wale waliozoea kuishi kama malaika sasa wajiandae kuishi kama shetani.
Rais Magufuli mwenyewe alitangaza katikati ya wiki kuwa anapokea Sh. milioni 9.5 kwa mwezi, kiwango ambacho ni chini ya mshahara wa wabunge wa Sh. milioni 11.9 kabla ya makato.
Akiwa mapumzikoni mkoani Geita katikati ya wiki, Rais Magufuli alisema atapunguza mishahara mikubwa wanayolipwa wakuu wa taasisi za umma ili kuendana na dhamira ya serikali yake ya kujielekeza zaidi katika kuinua hali za wananchi na kwa kufanya hivyo, wale waliozoea kuishi kama malaika sasa wajiandae kuishi kama shetani.
No comments:
Post a Comment