Dar es Salaam. Ripoti ya utafiti kuhusu ujangili wa meno ya tembo imebaini kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi mbili za Afrika ambazo idadi kubwa ya tembo wanauawa.
Utafiti huo wa njia ya vinasaba (DNA) uliofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC), Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol) ulibaini kuwa asilimia 85 ya meno ya tembo yanayokamatwa asili yake ni mbuga za Selous, Ruaha na Ruangwa, Tanzania.
Kadhalika, utafiti huo umebaini kuwa nchi nyingine ambayo tembo wengi wanauawa ni Congo.
No comments:
Post a Comment