POLISI WASIOWAPIGIA SALUTI WABUNGE KUKATWA MSHAHARA

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Fakharia Khamis amehoji bungeni adhabu gani askari anapewa ikiwa atashindwa kutoa saluti kwa mbunge.

 Katika swali la nyongeza mbunge huyo alitaka kujua maana ya saluti kwa askari ni nini, na viongozi gani wa uraiani wanaotakiwa kupigiwa saluti katika mhimili wa Bunge, Serikali na Mahakama.

Akijibu swali la mbunge huyo, Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole Nasha kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi alisema Serikali imetangaza adhabu ya kuwakata mishahara na adhabu nyingine, askari polisi wote nchini ambao hawatawapigia saluti wabunge wa Bunge la Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Ole Nasha alisema kumpigia saluti mbunge ni jambo la lazima kwa askari kwa kuwa lipo kwenye moja ya masharti yao, hivyo kutokufanya hivyo ni kushindwa kutii kiapo cha uaminifu wao.

No comments:

Post a Comment