Ni katika muktadha huo, bwana mmoja ambaye nimekuwa nikiona maandishi yake kwenye mitandao kwa jina la Malisa G. J, hivi karibuni aliandika maoni yake kuhusu hali ya uchumi kwa jinsi anavyoiona yeye, lakini akaacha pendekezo linalotaka ikiwezekana tuendelee kucheka na manyani hata kama tunavuna mabua! Kimsingi alikuwa anaangalia hatua anazochukua Rais John Magufuli za kubana matumizi, kupambana na ubadhirifu pamoja na ufisadi, na kuelezea faida zake na hasara zinazoweza kujitokeza kwa mtazamo wake.
Akamalizia hoja zake kwa kusema: “Sisemi Rais aendelee kubana matumizi au aache. Nachotaka kusema ni kuwa apime kati ya faida na hasara kisha afanye maamuzi kwa maslahi ya nchi...” Kwanza nianze kwa kuheshimu uchambuzi wake ambao kwa sehemu kubwa ni mzuri, lakini mgogoro wangu uko kwenye hitimisho lake.
No comments:
Post a Comment