
Mkuu wa Wilaya ya Longido, Daniel Chongolo amethibitisha kutokea tukio hilo juzi akisema amefanya mazungumzo na wanawake hao na kufikia mwafaka.
Chongolo amesema kuwa hoja za wanawake hao ilikuwa ni waume zao kila wanapopata fedha wamekuwa wakiondoka nyumbani na kuvuka mpaka na kuingia nchini kufanya starehe na baadhi yao wamelowea katika miji ya Namanga na Longido.
“Kwanza kabla ya kuwasikiliza niliwaeleza wamevunja sheria kwa kuingia nchini na kufanya vurugu... walikiri na kuomba radhi,” alisema Chongolo.
Amesema Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo, imeagiza wote walioharibiwa mali kutokana na maandamano hayo kufanya tathimini na kutoa taarifa ya hasara waliyopata.
No comments:
Post a Comment