KILIMANJARO WAADHIMISHA MIAKA 17 YA KUMBUKUMBU CHA KIFO CHA BABA WA TAIFA KWA KUOTESHA MITI.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Said Meck Sadiki akiongozana na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) Joyce Msiru wakati alipowasili katika chanzo cha maji cha Shiri kwa ajili ya zoezi la kuotesha miti ikiwa ni kuadhimisha miaka 17 ya kifo cha Baba wa Taifa ,Hayati Mwl Julius Nyerere.
Wakuu wa wilaya za Hai na Moshi ,Gelasius Byakanwa (wa pili toka kulia) na Kippi Warioba (wa tatu toka kushoto waliungana na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro katika zoezi hilo.kulia ni Katibu tawala wa mkoa wa Kilimanjaro Mhandisi Aisha Amour.

No comments:

Post a Comment