Jumla ya askari 152 wamefukuzwa kazi mwaka huu na Jeshi la Polisi kwa sababu ya kukiuka Sheria, Taratibu na Kanuni ya Jeshi hilo kama zilivyoainishwa katika Kanuni za Kudumu za Polisi (PGO) namba 103.
Idadi ya askari hao waliofukuzwa kazi imetolewa jana mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Maryam Msabaha aliyehitaji kufahamu juu ya idadi ya askari waliochukuliwa hatua kwa sababu ya utovu wa nidhamu.
Mhandisi Masauni alisema kuwa kazi ya Vikosi vya Ulinzi na Usalama ni kulinda raia, mali zao pamoja na mipaka ya nchi lakini kuna baadhi ya askari hao wanakwenda kinyume na Sheria kwa kuwapiga wananchi na kuwasababishia ulemavu pamoja na vifo hivyo Jeshi hilo limewachukulia hatua za kinidhamu.

No comments:
Post a Comment