WAMACHINGA JIJINI DAR ES SALAAM WAMPONGEZA RAIS DK.JOHN MAGUFULI KWA KUWARUHUSU KUFANYABIASHARA BILA KUBUGUDHIWA

Wauza mitumba katika Soko la Tandika wakiwa wamepozi kwa furaha baada ya Rais Dk.John Magufuli kuwaruhusu kufanya biashara zao pasipo kubugudhiwa.

Na Dotto Mwaibale
WAFANYABIASHARA ndogo ndogo wa Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam wamempongeza Rais Dk.John Magufuli kwa kuwaruhusu kuendelea kufanyabiashara zao bila ya kubugudhiwa na kumtaja kuwa ni kiongozi wa wanyonge na watu wa chini.

Kauli hiyo wameitoa leo asubuhi wakati wakitoa maoni yao baada ya Rais kutoa tamko hilo Dar es Salaam jana.

Mchuuzi wa urembo katika Soko la Tandika Kamtanda Hamisi alimshukuru rais kwa kuwaruhusu na kuwajali watu wa chini.

"Nawaomba wafanyabiashara wenzangu ruhusa ya rais isiwe kibali cha sisi kuanza kupanga biashara zetu barabarani tufuate sheria" alisema Hamisi.

No comments:

Post a Comment