Wenye mabasi kuanza kutumia EFDs


MAMLAKA ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), Mkoa wa Mbeya, imewataka wamiliki wa mabasi ya abiria kwenda mikoani na wilayani, kuhakikisha wanawasilisha taarifa za mabasi yao ili ziingizwe kwenye mitandao kwa matumizi ya tiketi za mfumo wa kielektroniki.

Taarifa hiyo ilitolewa jana na Ofisa Mfawidhi wa Sumatra, Mkoa wa Mbeya, Denis Daudi, alipokuwa akizungumza na MTANZANIA.

Katika utekelezaji wa mpango huo, Daudi alisema wameshaingia mkataba na kampuni moja binafsi itakayofanya kazi ya kusajili mabasi na kuingiza taarifa zake kwenye mitandao kwa ajili ya matumizi ya mfumo wa mashine za kielektroniki ziitwazo EFD.

“Mfumo huo hautofautiani na mfumo unaotumiwa na makampuni ya ndege na zoezi hilo linatarajia kuanza rasmi wakati wowote kuanzia sasa.

“Malipo yote yatafanyika kwa njia ya mtandao kwani mpango huo utapunguza usumbufu mkubwa waliokuwa wakiupata abiria wakati wa kukata tiketi.

No comments:

Post a Comment