Wanufaika mishahara hewa waanza kubanwa

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Angela Kairuki
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Angela Kairuki

SAKATA la mishahara hewa iliyokuwa ikiigharimu Serikali zaidi ya Sh bilioni 1.8 kila mwaka, limechukua sura mpya baada ya mishahara hiyo kubainika kuwepo karibu katika kila kona ya nchi.

Mbali na kusababisha aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango kusimamishwa kazi kabla hata ya kumaliza mwezi tangu aanze kutumikia cheo hicho, sasa watumishi walionufaika na mishahara hiyo wameanza kushikwa na kufikishwa mahakamani.

Jana, Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Imani Abdul, maarufu kwa jina la Nyamangaro (44), alipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Singida, akikabiliwa na makosa ya wizi wa mishahara ya watumishi hewa inayofikia Sh milioni 29.4.

No comments:

Post a Comment